“Nampongeza sana Bw. Francisco kwani amekuja na ubunifu mkubwa ambao unaendea kutatua changamoto kwa watoa huduma za afya hapa Muhimbili vilevile ubunifu huu utaenda kunufaisha watoa huduma wa afya katika hospitali zingine nchini” amesema Prof. Janabi.
Awali akizungumza kabla ya kukabidhi kitanda hicho Bw. Francisco amesema kuwa alipata wazo la kutengeneza kitanda hicho baada ya kuona changamoto wanazokutana nazo watoa huduma wakati wa kumshusha mgonjwa kutoka kwenye gari na kumpelekea wodini.
“Changamoto iliyonifanya nibuni kitanda hiki ni pale mgonjwa anaposhushwa anaweza kupata maumivu makali wakati wa kumshusha kutoka kwenye gari la wagonjwa na kumuweka kwenye kitanda cha nje pia wakati mwingine mgonjwa anaweza kudondoka” amesema Bw. Francisco
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...