Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amekutana na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Qatar, Mhe. Mohammed bin Ali  Al Mannai na ujumbe wake kando ya ukumbi wa mkutano Hoteli ya Sheraton Grand Doha, Qatar leo tarehe: 11 Desemba 2023.

Katika mazungumzo yao wamegusia ushirikiano na kubadilishana uzoefu katika nyanja mbalimbali za sekta ya mawasiliano na teknolojia ya habari ikiwemo masuala yanayohusu uchumi wa kidijitali kwa maeneo watakayokubaliana kupitia mkataba wa makubaliano (MOU)  ambao utaleta mageuzi ya mifumo ya kidijitali utakaoshirikisha Serikali ya Qatar na Tanzania.

Katika kikao hicho wamezungumzia mifumo ya kodi kwa njia za kidijitali kupitia sekta ya Utalii, Huduma za Afya na mapambano dhidi ya rushwa. 

đź—“️11 Desemba 2023

📍Hoteli ya Sheraton Grand, Qatar.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...