--Royal Tour yatajwa kuwa chanzo

Kaimu Kamishna wa Uhifadhi kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Juma Kuji amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani baada ya uzinduzi wa filamu ya ‘Royal Tour’ kumekuwa na mafuriko ya watalii katika maeneo tofauti ya hifadhi nchini.

Kuji ametoa kauli hiyo mara baada ya kuibuka Mshindi wa pili katika Tuzo za Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) zilizofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo amesema kuwa imepelekea kuwepo kwa ongezeko kubwa la wageni na hivyo kukuza Pato la Taifa.

Akizungumzia ushindi waliopata TANAPA amesema kuwa ni chachu kwao kama Shirika na inaonesha wazi kwamba utoaji wa taarifa za fedha na utunzaji kumbukumbu hivyo Watanzania waendelee kuwa na imani na TANAPA kwa kutembelea hifadhi zilizopo nchini.

“Mwaka huu tumeibuka mshindi wa pili, mwakani tutahakikisha tunakuwa nambari moja kwani uwezo na nia tunayo ya kusimamia vizuri Maliasili za taifa”, amesema Kamishna Kuji.

“Watanzania watumie mapumziko ya mwezi Disemba kutembelea vivutio vilivyopo katika maeneo mbalimbali nchini, TANAPA tupo vizuri katika utoaji taarifa na utunzaji vitabu”, amesisitiza Kuji

Tuzo za uandaaji wa taarifa za fedha kwa mwaka 2023, ambazo huandaliwa na Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) zimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya APC jijini Dar es Salaam.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...