


Ofisa Mkuu wa Uhusiano EWURA, Bw. Wilfred Mwakalosi, akiwasilisha mada kuhusu Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji, wakati wa semina iliyoandaliwa na EWURA kwa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Sheria Ndogo,iliyofanyika bungeni jijini Dodoma.



..........
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imeendesha semina ya siku moja kuhusu Udhibiti kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo, chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Jasson Rweikiza.
Akiwasilisha mada kuhusu kazi na majukumu ya EWURA, Ofisa Mkuu wa Uhusiano, Bw. Wilfred Mwakalosi, alisema EWURA ina jukumu kuu la kuhakikisha huduma zinazodhibitiwa zinapatikana kwa wakati na kwa gharama sahihi.
Akijibu hoja kuhusu masuala ya petroli kwenye semina hiyo, Mkurugenzi wa Idara ya Petroli Bw. Gerald Maganga alisema EWURA iko mbioni kuanza kuwianisha gharama za mafuta kwa bandari zote zinazopokea mafuta nchini ili kuongeza tija.
Semina hiyo pia imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga na viongozi wengine kutoka Wizara ya Nishati na EWURA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...