Na Mwandishi Wetu

MEYA wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Pascal Kihanga, ameomba,  wadau, taasisi na  mashirika kuendelea  kutoa misaada kwa wa athirika wa mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha mkoani humo.

Amesema mvua hiyo pia  imelazim Shule ya Sekondari Juhudi  iliyopo katika halmashauri hiyo kufungwa kutokana na kuzingirwa na maji  na kufanya uongozi  kutafuta eneo lingine  la kujenga shule hiyo.

Meya Kihanga amesema kata nne  za Lukobe,  Kihonda, Mkundi  na  Mazimbu, zimeathirika kwa kiasai kikubwa na mafuriko hayo.

Ametaja  kata zingine  zilizoathiriwa na mvuaa hiyo ni  Mindu na Bigwa ambazo licha ya kutokuaathirika sana lakini  misaada ya hali na mali  inahitajika.

 “Kuna  hali ngumu   kwa wananchi katika maeneo hayo. Nyumba  nyingi  zimebomoka, zimeingiliwa  na maji na kusomba   mali  za wananchi. Wengi hawana paa kuishi, chakula na mavazi,”amesema  Meya Kihanga.

Ameeleza, kutokana athari hizo  hatua mbalimbali  zimechukuliwa na serikali ya mkoa,wilaya  na halmashauri hiyo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wananchi waliokosa mahari pa kuishi  wanahifadhiwa, kupatiwa chakula na mavazi.

“Sisi mpaka sasa tumeanza kutoa misaada mbalimbali  kwa uwezo wetu. Ninaiomba jamii, ituangalie Morogoro kama  inavyo ziangalia sehemu zingine zilizoaathiriwa na mafuriko. Tunahitaji misaada,”amesema.

Amebainisha mahitaji  yanayohitajika zaidi ni chakula, mavazi, magodorona mashuka na misaada  yote ikabidhiwe Ofisi ya Mkuu  wa Wilaya ya Morogoro.

Amesemaa misaada inapokelewa kutoka kwa mtu yoyote, mkoa wowote na hata akiwa na mavazi mazuri yaliyovaliwa.
Meya Kihanga, amewataka wananchi kuendelea  kuchukua tahadhari  hasa  wakati huu  mvua inapoendelea  kunyesha.

“Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imekuwa ikitoa tahaadhari ya  kuwepo kwa mvua zaidi. Wananchi  wachukue tahadhari.Pia walinde watoto na kuto kudharau nguvu ya maji,”ameeleza  Meya Kihanga.


Ameishukuru  Serikali  hususan  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Jenista Mhagama, ambaye  amekuwa mstari wa mbele kushughulikia athari hizo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...