Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, leo Januari 22, 2024, ameshuhudia hafla ya utiaji wa Saini Mikataba 7 yenye Thamani ya Bilioni 2.3.

Mikatabia hiyo itahusisha ujenzi wa lami, ujenzi wa barabara za changarawe, madaraja na matengenezo maalumu katika mtandao wa barabara zinazohudimiwa na TARURA Mkoani Manyara.

Akizungimza kwenye hafla hiyo RC Sendiga, ametoa maelekezo kwa wakandarasi kuhakikisha wanatekeleza miradi hiyo sawa na vigezo na masharti ya mkataba na kuzingatia ubora.
RC Sendiga, amewataka wakandarasi hao kuwapa kipaumbele cha ajira wazawa wa Mkoa wa Manyara, Vikundi vidogo vidogo vya vijana na wanawake ili waweze kukuza vipato vyao.


Mwisho RC Sendiga, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za kuboresha miundombinu ya barabara vijijini ambazo baadhi zimeharibiwa na mvua za masika zinazoendelea kunyesha Mkoani hapa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...