Mtoto Khalfan Gideon wa mkoani Kigoma leo Januari 28, 2024 amefikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma - Maweni na kuanza kupatiwa matibabu.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Maweni Dkt. Stanley Binagi amesema uchunguzi wa awali unaonesha chanzo cha ugonjwa wa Khalfan kimeanzia katika genetics tangu akiwa tumboni.

Amesema kwa sasa wamenza kumpatia tiba za awali mtoto huyo wakati wanafanya utaratibu wa kuchukua sampuli za ngozi kwa ajili kuotesha ili kujua undani wa tatizo na hatimaye kumpatia tiba stahiki.

Mapema hii leo, Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye amefika hospitalini hapo kumjulia hali mgonjwa huyo na kuwaagiza madaktari kuchukua hatua za haraka katika matibabu yake ili aweze kurudi shule kuendelea na masomo.

Tunalishukuru Shirika la Habari Tanzania (TBC) kwa kuonesha picha ya video ikimuonesha mtoto Khalfan Gideo akiomba msaada wa matibabu kwa Rais Samia Suluhu Hassan na Rais.

Wizara inatoa wito kwa jamii kuwapeleka watoto wenye changamoto za kiafya mapema Hospitalini kwa ajiili ya kupata matibabu na kutowafungia ndani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...