Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam 
KAMPUNIya Michezo ya Kubashiri ya Sportpesa na Kampuni ya Mtandao wa Simu ya Vodacom wamekuja na mchongo mpya kupitia huduma zao ambazo zitawawezesha wateja kubashiri michezo mbalimbali ya soka na kujishindia kiasi cha fedha.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano, Sportpesa, Sabrina Msuya amesema kupitia Supa Jackpot ya Sportpesa, wateja waweza kubashiri na kuwa Mabilionea kupitia mtandao wa Vodacom kupitia huduma ya M-PESA.

Sabrina amesema wateja watapata unafuu wa kubashiri michezo yao Sportpesa kupitia Vodacom na kushinda kiasi cha zaidi ya Shilingi Bilioni 1 endapo utafanikiwa kushinda michezo yote 17 ya Supa Jackpot au kushinda bonasi endapo mteja atabashiri na kushinda zaidi ya michezo 12 hadi 16 kwenye Jackpot.

Kwa upande wao Vodacom wamesema mteja anaweza kubashiri michezo yake ya Supa Jackpot ya Sportpesa kwa kupiga menu ya *150*00# na kuchagua 4 lipa kwa M-PESA, chagua 8 michezo ya kubashiri na chagua 7 Supa Jackpot.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...