Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimeendesha semina kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) leo tarehe 27 Januari, 2024 jijini Dodoma.

Semina hiyo imelenga kuwapa uelewa Wabunge wa Kamati ya PIC juu ya Uwekezaji na mwenendo wa sekta hiyo nchini pamoja na kufahamu mikakati mbalimbali inayotekelezwa na TIC katika kuimarisha sekta hiyo na kuhamasisha zaidi uwekezaji.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe Deus Clement Sangu (Mb), ameipongeza TIC kwa kuendesha semina hiyo iliyotoa fursa kwa wajumbe hao kufahamu zaidi juu ya uratibu wa uwekezaji nchini na kufahamu kwa hali halisi ya uwekezaji, malengo, fursa na changamoto zinazoikabili sekta hiyo.

Mwenyekiti wa Bodi ya TIC, Dkt. Binilith Mahenge, amewapongeza wajumbe wa Kamati ya PIC kwa kazi nzuri wanayofanya na ushirikiano wanaoutoa katika kusaidia kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya TIC.

Semina hiyo pia imehudhuriwa na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Uwekezaji- Sekta Binafsi wa Wizara ya Ndg. Fadhili Chilumba na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya TIC ambao ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Ndg. Shani Mayosa, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha, Ndg. Pascal Maganga na Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji Ndg. John Mnali.
 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji  ya Umma (PIC) Deus Sangu akizungumza katika Semina iliyoandaliwa na TIC kwa Wabunge wa Kamati hiyo  iliyofanyika jijini Dodoma.
 

Mwenyekiti wa bodi ya TIC Dkt. Binilith Mahenge akizungumza wakati wa semina kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC)iliyofanyika jijini Dodoma.
 

Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji -TIC  John Mnali  akitoa maelezo kuhusiana na uhamasishaji wakati  wa semina kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) iliyofanyika jijini Dodoma.
 

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Uwekezaji- Sekta Binafsi kutoka Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji  Fadhili Chilumba akitoa mada  wakati  wa semina kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) iliyofanyika jijini Dodoma.
 

Baadhi ya matukio ya Picha katika Semina ya Kamati ya Bunge iliyoratibiwa na TIC

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...