Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar mpya itakuwa na usafiri wa umma wa mabasi ya umeme, treni pamoja na Taxi za baharini.

Amesema Serikali itatiliana saini mradi wa kituo cha usafiri wa baharini eneo la Mpiga Duri tarehe 09 Januari 2024.

Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo alipoweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Soko kuu la Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi B , Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe: 06 Januari 2024 katika shamrashamra za Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Aidha Rais Dkt.Mwinyi amesema ametimiza ahadi aliyoitoa kwa wafanyabiashara wakati wa kipindi cha kampeni za uchaguzi Mwaka 2020 ikiwemo kuwajengea mazingira bora ya kufanyia biashara, kuwawezesha kwa mitaji na vitendea kazi.

Vilevile ameeleza Serikali imetimiza ahadi yake kwa kutoa mikopo inayofikia bilioni 25 kuwawezesha wajasiriamali nchini na halikadhalika wavuvi, wakulima wa mwani wamepatiwa boti bila kuwasahau waendesha bodaboda.

Halikadhalika Rais Dkt.Mwinyi ametoa kipaumbele kwa wafanyabiashara wa awali wa soko la Mwanakwerekwe baada ya kukamilika Mwezi Machi kati ya wafanyabiashara 5,000 watakaoingia kwenye soko hilo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...