Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akisalimiana na Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi (majenerali wastaafu) nchini, wakati wa shughuli ya kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa marehemu Luteni Jenerali (mstaafu) Balozi Martin Nikusubula Mwakalindile, iliyofanyika Ijumaa, Februari 2, 2024, katika Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo, jijini Dar Es Salaam, kuanzia kushoto ni Jenerali Robert Mboma, Jenerali George Waitara, Jenerali Davis Mwamnyange na mwishoni kulia ni Jenerali Venance Mabeyo na nyuma yake ni Ndugu Abbas Mtemvu, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar Es Salaam (mwenye kofia).
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akitia saini kitabu cha maombolezo wakati wa kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa marehemu Luteni Jenerali (mstaafu) Balozi Martin Nikusubula Mwakalindile, katika Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo, jijini Dar Es Salaam, Februari 2, 2024. 
Rais Mstaafu, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akizungumza jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Jacob John Mkunda wakati kiongozi huyo alipoongoza waombolezaji wengine kushiriki shughuli ya kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa marehemu Luteni Jenerali (mstaafu), Balozi Martin Nikusubula Mwakalindile, iliyofanyika Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), leo Ijumaa, Februari 2, 2024. Kulia katika picha ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Stergomena Lawrence Tax na kushoto ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwapatia mkono wa pole familia ya Luteni Jenerali (mstaafu) Balozi Martin Nikusubula Mwakalindile wakati wa shughuli ya kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa marehemu Luteni Jenerali Mwakalindile, iliyofanyika katika Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo, jijini Dar Es Salaam, Ijumaa Februari 2, 2024.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akizungumza jambo na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Stergomena Lawrence Tax (Mb), wakati wa shughuli ya kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa marehemu Luteni Jenerali (mstaafu) Balozi Martin Nikusubula Mwakalindile, iliyofanyika Ijumaa, Februari 2, 2024, katika Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo, jijini Dar Es Salaam. Katikati yao ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Jacob John Mkunda.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akitoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa marehemu Luteni Jenerali (mstaafu) Balozi Martin Nikusubula Mwakalindile, katika Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo, jijini Dar Es Salaam, Ijumaa Februari 2, 2024.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...