NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulurhaman Kinana amekutana na Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika msiba wa Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Ngoyai Lowasa nyumbani kwake Osyesterbay Jijini Dar es Salaam

Jumanne Februari 13, 2024 mwili wa Hayati Lowasa unatarajiwa kuangwa na viongozi na wananchi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Jumatano Februari 14 mwili wa Hayati Lowasa utapelekwa katika Kanisa la KKKT Azania Front kwa ajili ya ibada takatifu na kuaga.

Alhamisi Februari 15 mwili wa Hayati Lowasa utasafirishwa hadi jijini Arusha ambapo viongozi na wananchi watapata fursa ya kuaga katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid.

Waziri Mkuu huyo mstaafu alifariki jana (Jumamosi, Februari 10, 2024) wakati akipatiwa matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam na tangazo la kifo chake lilitolewa na Makamu wa Rais Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...