Mwenyekiti wa taasi ya maisha bora (ZMBF) na mke wa rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Mama Mariam Mwinyi ameishauri wizara ya afya Zanzibar kuunda kamati ya lishe ya taifa ili kukabiliana na tatizo la utapiamlo.

 Mama Mwinyi ameongea hayo katika mkutano wa wadau wa lishe ulioandaliwa na taasisi ya maisha bora foundation – ZMBF inayotekeleza mradi wa lishe. 

 

ZMBF Imetoa vitendea kazi mbalimbali kwa wahudumu TISINI wa afya ngazi ya jamii wa visiwa vya PEMBA na UNGUJA ili wawafikie wananchi kwa urahisi na kukabiliana na tatizo la lishe.

 

Imebainishwa  katika mkutano huo kuwa upungufu wa damu unaosababishwa na lishe duni ni chanzo vya vifo vya mama na mtoto visiwani Zanzibar, imebainishwa 

 

Mkurugenzi wa kinga na elimu ya afya wa wizara ya Afya Zanzibar, Dkt. Salim Slim, amesema tathmini iliyofanywa na Wizara hiyo imebaini  asilimia 65.9 ya wanawake na watoto Zanzibar wana tatizo la lishe duni na upungufu wa damu hali inayo sababisha vifo vya uzazi.

 

Mradi wa lishe unaotekelezwa kwa ushirikiano wa ZMBF, taasisi ya BENJAMIN MKAPA - MBF na wadau wa lishe umeendelea kuhamasisha lishe bora kwa kutoa elimu kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii na tayari imewafikia zaidi ya wananchi  26,000 visiwani Zanzibar.

 

Naibu waziri wa  afya Zanzibar Hassan Khamis Hafidh na mjumbe wa bodi wa ZMBF na Naibu Spika wa baraza la wawakilishi Zanzibar Mhe. Mgeni Hassan Juma wamesema kuna haja serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ya kuongeza   bajeti ya lishe ili kukabiliana na vifo vya mama na mtoto.





Naibu Spika wa baraza la wawakilishi Zanzibar Mhe. Mgeni Hassan Juma akiongea katika mkutano huo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...