Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Sportpesa, Abbas Tarimba (wa kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya kiasi cha Tsh. 265, 780, 681 kwa mshindi wa Supa Jackpot ya Sportpesa, David Mwenge, ambaye alibashiri michezo 13, hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika jijini Dar es Salaam.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMPUNI ya Michezo ya Kubashiri ya Sportpesa inajivunia kuendelea kuchangia sehemu ya pato la taifa baada ya wateja wake kubashiri michezo mbalimbali na kushinda kiasi cha fedha ambacho kinachangia kodi ya taifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kukabidhi kiasi cha zaidi ya shilingi Milioni mbili (Tsh. 265, 780, 681) kwa mshindi wa Supa Jackpot, David Mwenge - Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Sportpesa, Abbas Tarimba amesema katika kiasi hicho cha fedha, Serikali imepata kodi yake asilimia 10.

Tarimba amesema Sportpesa imeendelea kuchangia fedha nyingi zaidi kila mwezi kupitia michezo hiyo ya kubashiri na kuendelea kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa la Tanzania. “Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanasema sisi Sportpesa ni walipaji wakubwa wa kodi,” amesema Tarimba

Aidha, Tarimba amesema licha ya kuchangia kodi kwa taifa na ukuaji wa uchumi kwa ujumla, kupitia michezo hiyo ya kubashiri na baada ya washindi kupatikana, vijana wengi wameendelea kupata ajira, kuweka akiba benki na baadae kupata faida na kubadilisha maisha yao.

Kwa upande wake, Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, Rasul Masoud amewapongeza Sportpesa kufika hatua hiyo ya kuwa walipaji wakubwa wa kodi kwa taifa, kukuza uchumi kupitia michezo hiyo ya kubashiri pamoja na kuinua hali za Watanzania wa kada mbalimbali.

Naye, Mshindi wa Supa Jackpot ya Sportpesa, David Mwenge amesema alianza kubashiri na Sportpesa tangu mwaka 2018 ambapo amekuwa akishinda kiasi cha fedha (Bonus) baada ya kubashiri michezo mbalimbali, Mwenge amesema hakupata usingizi alipopata ujumbe kuwa ameshinda kiasi cha fedha, Tsh. 265, 780, 681.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...