Kamati ya Kudumu ya Bunge, Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Deudatus Mwanyika leo tarehe 14 Machi, 2024 Imepokea na Kujadili Taarifa ya Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), inayohusu Utekelezaji wa Bajeti ya Maendeleo ya Kiwanda cha Kutengeneza Mashine na Vipuri (KMTC) kwa mwaka wa Fedha 2023/2024.

Kiwanda cha KMTC kilichopo katika Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, kimejikita katika uzalishaji wa mashine mbalimbali zikiwemo mashine za kukata na kuchonga, kufua chuma, kuranda mbao, pampu pamoja na vipuri. Lengo kuu la Kiwanda hiki cha KMTC ni kuwa mzalishaji wa mashine za viwandani ili kujenga na kukuza viwanda nchini. Kiwanda hiki kina maeneo makuu ya uzalishaji ambayo ni eneo la karakana ambapo shughuli kuu inayofanywa katika eneo hili ni uchongaji wa vipuri mbalimbali pamoja na kuunda mashine.

Aidha, kiwanda hiki cha KMTC kina vitengo mbalimbali vya uzalishaji ambapo kitengo cha Uundaji kazi yake ni kuunda maumbo na kuunganisha ili kupata mashine. Kitengo kingine ni cha uyeyushaji wa chuma na utengenezaji wa maumbo mbalimbali pamoja na kitengo cha uwekaji utando kwenye chuma ili kisipate kutu.

Hata hivyo, Mhe. Mwenyekiti pamoja na Waheshimiwa wajumbe walimpongeza sana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi anavyoendelea kufufua viwanda hususani kiwanda cha KMTC ambacho kilikuwa hakifanyi kazi kwa takriban miaka 29, pamoja na kutoa fedha za maendeleo katika kiwanda hicho. Mwenyekiti aliendelea kumshukuru Waziri wa Viwanda na Biashara kwa kusimamia vyema Uongozi pamoja na wafanyakazi wa kiwanda cha KMTC na kusisitiza kutafuta mali ghafi kwa wingi ili kuendelea kuzalisha vifaa hivyo na si kusubiri mteja mmoja mmoja.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...