Na Yeremias Ngerangera....Namtumbo.
 
Wakiongea katika mkutano wa hadhara wa Kijiji hicho ,wananchi wa Kijiji Cha Mdwema walisema wanaridhia Mpango wa matumizi Bora ya ardhi ya Kijiji Chao.

Greyson Choma ni mwenyekiti wa Kijiji Cha Mdwema Pamoja na kuwashukuru wananchi wa Kijiji chake kuridhia kupitisha Mpango wa matumizi Bora ya ardhi ya Kijiji Chao , aliwashukuru zaidi wafadhili  CARITAS waliogharimia Mpango huo .

Choma Pamoja na shukrani hizo aliwataka wananchi wa Kijiji hicho kufuata sheria,kanuni,miongozo na taratibu zilizowekwa katika kusimamia Mpango wa matumizi Bora ya ardhi .

Faustin Chuma mwananchi wa Kijiji Cha Mdwema Pamoja na kuridhia kupitisha Mpango huo aliiomba idara ya ardhi kupanda mawe kwenye mipaka kati ya Kijiji Chao na vijiji vingine ili kulinda ardhi Yao iliyotengwa Kwa ajili ya msitu ili wananchi wa vijiji vingine wasiingie katika maeneo hayo Kwa madai ya kutojua maeneo Yao.

Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Kelvin Mnali aliwaambia wananchi hao kuwa sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 inakataza kufanya shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji na maeneo ya milima huku akiwataka wananchi hao Kujua sheria hiyo katika kusimamia Mpango wa matumizi Bora ya ardhi ya Kijiji Chao.

Mary Albert Mratibu wa Mpango kutoka CARITAS ambao ndio waliofadhili Mpango huo alisema Kwa hatua za awali maeneo ya mipaka ya Kijiji hicho yatawekewa vibao kuonesha Shughuli inayotakiwa kufanywa katika eneo husika huku akiitaja idara ya ardhi ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo kuandaa ramani na kupanda mawe kuonesha mpaka wa Kijiji hicho na vijiji vingine.

Zakaria Kapinga Afisa ardhi mteule wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo aliwaambia wananchi wa Kijiji Cha Mdwema kuwa Mpango wa matumizi Bora ya ardhi ya Kijiji chao utakuwa wa Miaka kumi kuanzia mwaka huu 2024 mpaka mwaka 2034 na baada ya Miaka 10 Mpango huo unaweza ukafanyiwa mapitio.

CARITAS ni Taasisi isiyo ya kiserikali ambayo inajishughulisha na vikundi vya ufugaji wa Nguruwe na kilimo Cha mazao kupitia vikundi vidogo vidogo vya wakulima wa Kijiji Cha Mdwema ambapo Taasisi hiyo inatumia kiasi Cha shilingi milioni 12 kukifanya Kijiji hicho kuwa katika Mpango wa matumizi Bora ya ardhi yake ya Kijiji.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...