Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha.
WAKAZI
wa Kitongoji cha Kisabi , Mlandizi,Kibaha Vijijini , Mkoani Pwani
wanaotakiwa kupisha eneo hilo na kuhamia Kikongo eneo lenye ekari 1,000
lililotolewa na Serikali wamegomea kuhama wakidai ugumu wa kuanza maisha
mapya.
Hayo yalielezwa
na wakazi hao akiwemo Esther Shishima, Nuhu Msheka ,Daudi Mwasumbi
wakati Mkuu wa wilaya Kibaha Nikkison Simon alipomwakilisha Mkuu wa mkoa
wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge kwenye mkutano wa kusikiliza na kutatua
kero za wananchi.
Shishima aliiomba, Serikali kuwaacha waendelee kuishi katika eneo hilo kwani wamechoka kuhamahama na watoto kama wakimbizi.
"Tunaambiwa
tuhame kuwa kuna zuio la kimazingira tuache kuendelea kujenga,eti
sheria imekataa ,sasa mbona wapo wenzetu eneo la Halmashauri wanajenga
na wanamudu hiyo hali ,basi na sisi tutaweza,watuache tumechoka
kuhangaika na watoto" alifafanua Shishima.
Nae
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kisabi ,Yahaya Matata alieleza awali
waliovamia eneo hilo walikuwa 41 baadae wakaongezeka na kufikia 91 sasa
wameongezeka wapo zaidi ya 300.
Mkuu
wa wilaya ya Kibaha , Nikkison aliahidi kuyafikisha maombi hayo sehemu
husika kwa lengo la kutoa maamuzi zaidi ingawa alisisi kuwa kutokana na
ushauri wa kitaalam kimazingira eneo hilo si rafiki kwa makazi hiyo
wananchi wanapaswa kuhama.
Nikkison
alieleza Serikali ya mkoa ilitoa ekari 1,000 kwa wakazi wa Kisabi ili
lipimwe viwanja na kugawiwa kwa wakazi wanaoishi kwenye eneo Oevu.
Nikkison
alifafanua kuwa, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa mazingira-
NEMC lilitahadharisha juu ya eneo hilo kutumika kujengwa makazi ya
binadamu kwa kuwa ni oevu linaloweza kusababisha madhara yatokanayo na
mafuriko kikiwa ni pamoja na uwezekano wa nyumba kutitia.
Kutokana
na hali hiyo Ofisi iliamua kutafuta eneo rafiki linalofaa kwa makazi ya
binadamu ambalo alieleza linapatikana katika kijiji cha Kikongo na sasa
maandalizi ya upimaji unaendelea ili wakazi hao wapewe viwanja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...