NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

WANAJUKWAA wasichana kutoka vyuoni (Young Feminist Forum) wameiomba Serikali kutilia mkazo kwenye vipaumbele mbalimbali katika mwaka wa fedha ujao ambavyo ni vilio kwa jamii kubwa ya watu nchini kwa kutenga bajeti na kufanya ufatiliaji ili fedha zinazotengwa kufanya kusudi maalumu iliyopangiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 27,2024 katika ofisi za Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Mabibo-Dar es Salaam Mwanaharakati wa masuala ya jinsia Bi.Anna Sombe amesema wamejadili mambo katika suala la pembejeo za kilimo,bima ya afya,Mikopo ya Elimu ya vyuo vikuu,pamoja na miundombinu ya nishati na maji.

Aidha Bi.Anna amesema kwa upande wapembejeo za kilimo ambapo kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu zinatakiwa kufika kwa wananchi kwa wakati na kuondokana na desturi ya ucheleweshwaji ambao huchangia kuzorotesha uzalishaji wa mazao jambo ambalo linaendeleza njaa.

Pamoja na hayo Bi.Anna ameeleza kuhusina na suala la bima ya afya kwa watu wote kupewa kipaumbele kulifanya kuwa hitaji la lazima kwa watu kwa lengo la kuboresha afya za watu wote bila kujari hali zao za maisha.

Vilevile Bi.Anna amesema miundombinu ya nishati na maji ni jambo la msingi na ni hitaji la kila siku hivyo serikali inatakiwa kutilia nguvu masuala hayo ili kuboresha maisha ya wananchi.

"Serikali iweke nguvu sio kutenga bajeti tu ufuatiliaji na utekelezaji pesa imeweka kwaajili ya ujenzi mabomba je yamewekwa unakuta watu wanafanya upigaji au wanazitumia pesa vinginevyo"Bi Anna amesema.

Kwa Upande wake Mdau wa semina za Jinsia Bi.Raiyan khatib ameiomba serikali kutoa kipaumbele Cha huduma bure kwa mama na mtoto pamoja na tiba bure ya saratani ya mlango wa kizazi.

"Unakuta mzazi amefika kipindi Cha kujifungua kama vile anamnunua mtoto Kuna huduma kule anatakiwa alipe,Kuna vifaa anaambiwa toka nenda kanunie vifaa kwenye duka la nje"Bi.Raiyana amesema.











Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...