RAIS Samia Suluhu Hassan ameendelea kutajwa kupitia majukwaa mbalimbali kutokana na jitihada zake za kuboresha uchumi wa Taifa katika sekta mbalimbali na katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake amefanikiwa kuongeza fursa hasa za ushiriki wa sekta binafsi na kupanua wigo wa ukuaji wa uchumi nchini.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam leo na Mchambuzi wa Masuala ya Uchumi nchini, Prof. Samwel Wangwe wakati wa mdahalo maalum ulioandaliwa na kampuni ya Mchambuzi Media kwa lengo la kutathmini miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia.

Ameeleza kuwa, Rais Samia amejipambanua kama mlezi wa sekta binafsi na amekuwa na mikutano ya mara kwa mara na sekta hiyo ambayo inalenga kuwekana sana katika masuala ya kupanua wigo wa ukuaji wa uchumi na wanaoshiriki katika ukuaji huo.

"Pia Rais Samia amefanikiwa kuongeza uzalishaji na tija katika sekta ya kilimo, ameongeza mahusiano ya kiuchumi kuanzia nchi jirani hali iliyofanya wawekezaji kutoka nje kuongezeka na kusababisha uchumi kukua kwa kasi," amesema.

Pia amesema kati ya maeneo ambayo yalilega kiuchumi wakati Rais Samia anaingia madarakani ni pamoja na eneo la utalii ambalo alilitilia mkazo na kuongoza filamu ya Royal Tour iliyosaidia kuongezeka kwa watalii kutoka 700,000 hadi kufikia Milioni 1.8.

Kwa upande wake Mchambuzi wa Masuala ya Kisiasa, Kiuchumi, Kijamii, Kitaifa na Kimataifa, Dk. Denis Muchunguzi amesema katika kuangalia miaka hiyo mitatù ya uongozi wà Rais Samia ni muhimu kuundwa kwa tume au kuweka utaratibu ambao utawasaidia na kuwaongezea nguvu wakuu wa Mikoa ,Wilaya na Wakurugenzi kuwa na uwezo wa kutatua kero za wananchi.

“Tusisubiri mpaka aende Makonda kutatua kero, uwekwe utaratibu utakaowaongezea nguvu na uwezo kwa wakuu wetu wa mikoa,Wilaya na Wakurugenzi ili kuweza kusikiliza na kutatua kero za wananchi, " amesema Dk. Mchunguzi.

Aidha Mkurugenzi wa Kampuni ya Mchambuzi Media ambao ndio waandaaji wa mdahalo huo, Salehe Mohamed amesema mdahalo huo umelenga kuangalia maeneo ambayo Rais Samia amefanya vizuri na yale ambayo hajafanya vizuri na nini kifanyike kupiga hatua ili maisha ya watanzania yaendelee kuwa bora zaidi.

Amesema katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia amefanikiwa kuinua sekta ya kilimo ambayo katika miaka ijayo itaifanya nchi kuwa na uchumi imara zaidi.

"Rais amefanikiwa pia katika sekta ya elimu tumesikia wakati anaingia madarakani udahili wa wanafunzi ulikuwa haujafika hata 10,000 ila sasa hivi umefikia 17,000, eneo jingine ni sekta afya yaani sasa hivi karibu kila wilaya kama siyo Zahanati basi kuna hospitali kuna na vifaa vya kisasa ambavyo vinawafanya watanzania kupata matibabu kwa kiwango cha hali ya juu," amesema Mohamed.
Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF,) Bakari Machumu akichangia mada wakati wa jukwaa hilo lililofanyika jijini Dar es Salaam.


 

Matukio mbalimbali wakati wa jukwaa Hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...