Na Mwamvua Mwinyi,MBEZI Machi 15

Hii ni wiki ya maadhimisho ya Ugonjwa wa Shinikizo la macho au Presha ya Macho duniani ambapo hospitali ya CCBRT,kwa kushirikiana na hospitali ya Barrack PolisI Kilwa Road na halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, wameadhimisha kwa kutoa huduma ya upimaji macho kwa madereva wa mabasi yaendayo mikoani kwa lengo la kunusuru uoni wa macho yao kutokana na kazi muhimu wanayoifanya.

Pia huduma hii inatolewa kwa mtu yoyote anayefika kituoni hapo ambapo tangu kuanza kwa zoezi hilo la wiki moja tarehe 12.3.2024 zaidi ya watu 400 walikuwa wamepatiwa huduma.

Ugonjwa wa presha ya macho unatajwa na wataalamu wa afya ya macho duniani kuwa wa kwanza kusababisha upofu usiotibika duniani.






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...