Na Abel Paul, Jeshi la Polisi-Arusha.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Kimeendelea na operesheni ya kutoa elimu na kuwakamata wale wote wanaoendelea kuvunja sheria za usalama Barabarani huku Jeshi hilo likiwapongeza wale wote waliotii agizo la serikali la kuondoa namba ambazo hazijasibitishwa na mamlaka ya viwango Tanzania (TBS).

Akiwa katika Operesheni hiyo leo Machi 19, 2024 Mkoani Arusha Mkuu wa Operesheni za kikosi cha Usalama barabarani Nchini kamishna msaidizi wa Polisi ACP Nasoro Sisiwayah amesema kikosi hicho kinaendelea kuwakamata wale wote walio kaidi agizo la kuondoa namba zenye ujazo 3D na ving’ora.

ACP Sisiwayah ameongeza kuwa operesheni hiyo imelenga pia kukamata madeni ya wale wote waliofanya makosa barabarani na kupigwa faini ambapo amebainisha kuwa zoezi hilo linaendela nchi nzima huku akiwaomba watumiaji wa vyombo vya moto ambao wanadaiwa kuhakikisha wanalipa madeni yao kwa wakati.

Aidha amesema kuwa operesheni hiyo pia imehusisha kuwakamata wale wote wanaoendesha mwendo kasi vyombo vya moto ambapo amebainisha kuwa uchunguzi wa Jeshi hilo unapofanyika umebaini kuwa chanzo cha ajali nyingi ni mwendo kasi hivyo nao watakamatwa.

Nao baadhi ya madereva licha ya kupongeza operesheni hiyo wamebainisha kuwa undoshaji wa namba hizo utasaidia katika swala la ulinzi na usalama huku wakiliomba Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani kuendelea na operesheni hiyo ambayo itasaidia katika usalama.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...