Serikali kupitia Wakala ya Barabara (TANROADS) imeendelea kuufungua Mkoa wa Simiyu kwa kutekeleza zaidi ya miradi mikubwa mitano ya Kitaifa ya ujenzi wa Miundombinu ya Barabara na madaraja

Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Simiyu, Mha. Boniface Mkumbo ameyasema hayo alipozungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita katika sekta ya ujenzi.

Amesema Serikali kupitia TANROADS imefanikiwa kukamilisha ujenzi wa awamu ya tatu ya kipande cha barabara ya Bariadi-Maswa yenye urefu wa Km 49.7 pamoja na Barabara ya mchepuo ya Maswa ( Maswa Bypass) sehemu ya Lamadi-Bariadi-Maswa - Wigelekelo hadi Mwigumbi upande wa Shinyanga na Daraja la Malampaka lenye mita 12.5.

Amesema miradi mingine ambayo ipo kwenye utekelezaji wa kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami ni pamoja na Barabara ya Bariadi - Salama - Gh’aya- Magu (Km 76) ambayo itaunganisha mkoa wa Simiyu na Mwanza, Barabara ya Nyashimo - Ngasamo - Ndutwa (km 48), na mradi mkubwa wa ujenzi wa Barabara ya Karatu-Mbutu - Hydom - Mto Sibiti - Meatu - Lalago - Maswa yenye Jumla ya kilometa 339.

Amesema madaraja zaidia 20 yamejengwa katika mtandao wa barabara kwa gharama ya Shilingi Bilioni 5.6 na Ujenzi wa Daraja kubwa la Itembe lenye urefu wa mita 150 unaendelea ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 75 ambalo linaunganisha Mkoa wa Singida, Mikoa mingine ya Kanda ya kati na kanda ya kaskazini.

Amesema katika kipindi cha miaka 3 cha Serikali ya awamu ya sita zaidi ya taa 569 za barabarani zimefungwa kwenye miji na Vijiji vikubwa ili kuwafanya wananchi kuendelea na shughuli zao za kiuchumi na kijamii hata giza linapoingia.

Pia, ameishukuru Serikali kwa kuweza kuwajali Wakandarasi Wazawa ambapo Mkoa wa Simiyu ni Moja kati ya Mikoa ambayo kazi nyingi wamepewa Wakandarasi wa ndani na kuwapa Kipaumbele Wanawake ili kuweza kuwawezasha kupewa upendeleo ili kuwakuza kiuchumi.

Mha. Mkumbo ametoa wito kwa Wananchi kutunza Miundombinu ya Barabara kwani Serikali inatumia fedha kuhakikisha wananchi wanapita kwenye Miumbombinu iliyo na viwango vinavyokubalika.

Naye, Msimamizi wa idara ya Matengenezo TANROADS Simiyu, Mha. Amiri kwiro ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutenga fedha za matengenezo mkoa humo ambazo pia kwa kiasi kikubwa zimesaidia kuepuka madhara ya mvua za Elnino zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali Nchini.








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...