Na Mwandishi Wetu, Barcelona

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Ubalozi huo imesema kwamba maonesho hayo ya siku tatu yana lengo la kuwawezesha wenyeji wa Barcelona wenye wa asili ya Catalunya (Catalans) ambao wana desturi ya kutembelea kwa wingi maonesho hayo kutafuta maeneo ya kutembelea wakati wa majira ya kiangazi yanayokaribia kuanza.
Wakati wa ufunguzi, Waziri wa Biasahara na Kazi Roger Torrent i Ramio alitembelea banda la Tanzania na kushukuru kwa ushiriki wa Tanzania kwa kueleza Tanzania na Zanzibar ni maeneo yanayovutia watu wengi kuyatembelea kwa sasa na kwamba anategemea mafanikio makubwa ya Tanzania katika sekta ya utalii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...