Upendo ndiyo Nguzo ya Mafanikio yetu-Kikwete (MB) Maneno hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete alipokuwa anaongea na Viongozi wa Chama wa Halmashauri ya Chalinze alipowaalika kwenye Futari nyumbani kwake Msoga.

Futari hiyo iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama wilayani hapo akiwepo Mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo Ndg. Abdul sharif Zahor na wajumbe wa Halmashauri ya Wilaya kutoka kata zote za Jimbo la Chalinze ililenga kuwakutanisha viongozi wa wilaya ikiwa na malengo ya kuupokea mfungo wa mwezi wa Ramadhani, kuwaombea na kuwarehemu viongozi waliowahi kuongoza Wilaya hiyo na amani ya Wilaya hiyo na Wazee.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...