MFANYABIASHARA Marik Ngutti wa Machimbo ya Matabi wilayani Chato Mkoa wa Geita ameeleza namna ambavyo ufuatiliaji wake wa elimu ya mlipa kodi ilivyomnasua kutoka kwenye mikono ya matapeli waliojifanya maofisa Mamlaka ya Mapato (TRA).

Ngutti ametoa ushuhuda huo leo Aprili 23, 2024 alipotembelea banda la TRA katika maonesho ya Wakandarasi Geita Mjini kwenye viwanja vya EPZ ambapo amesema aliwapa elimu na wafanya biashara wenzake ambao pia walishindwa kutapeliwa baada ya kupata taarifa muhimu kuhusu maofisa wa TRA.

"Kuna watu walikuja kwenye maeneo yetu ya biashara pale Machimbo ya Matabi walijitambulisha kuwa ni maofisa wa TRA niliwajengea mashaka kwa kuwa niliona hawana utambulisho wa TRA na hawakuwa wanatoa lisiti kwa wenzetu waliotangulia kupita nikawaambia wafanyabiashara wenzangu kuwa hao sio maofisa wa TRA nikawapa namba ya TRA"

Amesema kwa kuwa tayari alishawapa elimu ya mlipa kodi walivyofika wale maofisa bandia wa TRA wale wafanyabiashara waliwahoji mambo muhimu yanayohusu TRA waliposhindwa kujibu wakaondoka zao na .

Ngutti amesema kuwa ufahamu juu ya masuala muhimu ya kodi na maofisa wa TRA ameyapata kutokana na jitihada zake za kufuatilia vipindi mbalimbali vya runinga na radio na kuwasisitiza wananchi wote kujielimisha katika masula muhimu ya kodi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...