Bingwa wa mchezo wa vishale (Darts) wanaume Omary Mmbaga kutoka wa timu ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (Ulinzi Sports Club) akionesha utaalamu wake wakati wa michuano ya Kombe la Mei Mosi Taifa 2024 inayoendelea Jijini Arusha.
Bingwa wa mchezo wa vishale (Darts) wanawake Scholastica Kaizer kutoka wa timu ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (Ulinzi Sports Club) akionesha utaalamu wake wakati wa michuano ya Kombe la Mei Mosi Taifa 2024 inayoendelea Jijini Arusha.

Na Mwandishi Wetu, Arusha
WACHEZAJI Omary Mmbaga na Scholastica Kaizer wa timu ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (Ulinzi Sports Club) wameibuka mabingwa wa mchezo wa vishale (darts) wa michuano ya Kombe la Mei Mosi Taifa 2024, uliofanyika Jijini Arusha.

Wachezaji hao wazoefu wamekuwa mabingwa wa kwanza katika mashindano hayo baada ya mchezo huo kuingizwa rasmi na kuchezwa kwa mara ya kwanza katika michuano hii,

Aidha, Mmbaga ni mzoefu wa mchezo huo ambapo amekuwa na mwendeleza mzuri wa kushinda katika michezo ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kwa miaka mitatu mfululizo, Michezo ya Mashirika ya Umma na Binafsi (SHIMMUTA) pamoja na masndano mengine.

Nafasi ya pili kwa wanaume imechukuliwa na Thomas Lemunge kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na nafasi ya tatu kwenda kwa Jerome Ndibalema kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Kwa upande wa wanawake nafasi ya pili imechukuliwa na Rehema Abdallah kutoka Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilfu Tanzania (TPHPA) na nafasi ya tatu imekwenda kwa Elizaberth Luwanda kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC).

Aidha, mchezo wa Netiboli umezikutanisha timu za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wamewafunga timu ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa magoli 34-31; nao TAMISEMI wamewachapa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) magoli 42-12.



Katika mchezo wa Kamba wanaume Idara ya Mahakama Tanzania imewavuta Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa mivuto 2-0, Ofisi ya Rais Ikulu wamewavuta Chuo cha Mipango kwa mivuto 2-0; kwa upande wa wanawake Wizara ya Afya wamewavuta Wizara ya UTamaduni kwa mivuto 2-0, Wizara ya Maji wamewavuta Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mivuto 2-0, Wizara ya Uchukuzi wamewavuta Wizara ya Fedha kwa mivuto 2-0 na Wizara Mambo ya Ndani ya Nchi imewavuta Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilfu Tanzania (TPHPA) kwa mivuto 2-0.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...