Kaimu Kaimu Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya UNESCO Tanzania Fatuma Mrope wa kwanza kutoka kulia akikabidhi cheti Mnufaifaika wa Ufadhili wa Masomo nchini Poland George Kato wa tatu kutoka kushoto katika makabidhiano yaliyofanyika katika Ofisi ya Tume hiyo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Kaimu Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya UNESCO Tanzania Fatuma Mrope wa kwanza kutoka kulia akikabidhiwa baadhi ya taarifa na Mnufaifaika wa Ufadhili wa Masomo nchini Poland George Kato wa tatu kutoka kushoto katika makabidhiano yaliyofanyika katika Ofisi ya Tume hiyo jijini Dar es Salaam.

*Miradi ya Kimkakati ni fursa ya kwenda kupata ufadhili na kuongeza maarifa

Na Chalila Kibuda,Michuzi Tv
VIJANA  nchini wametakiwa kuchangamkia fursa za kusoma nchi nchi zinazotolewa Tume ya Taifa ya UNESCO kutoka nchi wafadhili.

Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania imekuwa inapata ufadhili wa vijana katika kusoma nchi mbalimbali lakini changamoto iliyopo ni vijana kutoomba nafasi hizo za kusoma.

Hayo ameyasema Kaimu Katibu mtendaji mkuu wa Tume Fatuma Mrope amesema kuwa nafasi zipo nyingi za kusoma katika nchi za Poland ,China na nchi nyingine.

Amesema Teknolojia zinabadilika kila siku katika program za kusoma ambapo nchi ambazo zinatoa ufadhili zimefika mbalimbali ambapo kwenye miradi ya kimkakati inayofanyika nchini wanaweza kutumika kuliko kutafuta nje ya nchi hizo zilizoweza kuwa Teknolojia hizo na zikatoa ufadhili.

Kaimu huyo Fatma amesema kazi ya UNESCO ni kutafuta nchi zenye utayari wa kutoa ufadhili kwa vijana nchi za Afrika katika shahada ya kwanza,Shahada ya pili pamoja na shahada Uzamivu (PhD) na kuzitangaza kwa watanzania ili waweze kuomba na kunufaika nazo.

Akielezea utaratibu ulivyo Afisa Program wa UNESCO Tanzania Adrian Hyera amesema ufadhili unaotolewa ni bure na kazi kubwa kwa wanahitaji ni kuomba kwenye tovuti za Tume ya Taifa UNESCO Tanzania.

"Nchi nyingi fursa ufadhili wa kusoma wanazitumia zikifika Tanzania vijana hawaombi hadi program za nchi zilitoa ufadhili zinaisha"amesema Hyera

Aidha amesema kuwa ufadhili huo licha ya kuwa bure ni bure kwa kipindi unachokuwa unasoma na gharama zinazomhusu kama mwanafunzi ni kusoma tu.

Hyera amesema kuwa vijana wanaotaka kupata ufadhili nafasi ziko za kutosha kwani idadi wakati mwingine wanatakiwa 10 nchi lakini Tanzania unakuta hata kijana mmoja hajaenda.

Mmoja wa Wanufaika George Kato aliyekwenda kusoma utalii wa Miamba nchini Poland amesema kuwa kwa Tanzania alikuwa pekee yake huku baadhi ya nchi zikiwa zina zaidi ya watano.

Kato amesema kuwa haoni sababu ya vijana kushindwa kutumia fursa wakati kwao inaongeza utaalam wa kufanya kuingia katika ushindani wa soko la ajira.

Amesema kuwa wakati alipoenda ofisi za Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania alipata msaada mkubwa hadi kukamilisha taratibu na kwenda kusoma katika nchi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...