Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi kama ifuatavyo:

Amemteua Bw. Sylvester Joseph Kainda kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Bw. Kainda alikuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani.

Amemteua Bi. Eva Kiaki Nkya kuwa Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Bi. Nkya alikuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Amemteua Bw. Chiganga Mashauri Tengwa kuwa Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Bw. Tengwa alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Geita.

Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...