Katibu Siasa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo CCM mkoa wa Iringa, Joseph Ryata akiongea na walimu wazalendo wilaya ya Kilolo mkoani Iringa



Na Fredy Mgunda, Iringa

CHAMA cha Mapinduzi CCM mkoa wa Iringa kimewpongeza walimu wazalendo kufundisha kwa juhudi na kumuunga mkono Rais Dr Samia suluhu Hassan katika kutekeleza ila ya CCM ya 2020/2025 kwa vitendo.

Akizungumza na walimu wazalendo Katibu Siasa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo CCM mkoa wa Iringa, Joseph Ryata alisema kuwa walimu wamekuwa na mchango mkubwa wa kimaendeleo kutokana na kutoa elimu kwa wote na mara nyingine kuwaelimisha wazazi umuhimu wa elimu.

Ryata alisema kuwa walimu wanaaminiwa na jamii kutokana na elimu,burasa na maarifa wanayotumia kwa jamii wanayoishi nayo kwa kuwaelimisha mambo mbalimbali ya kimaisha na kimaendeleo.

Alitumia wasaa huo kuwataka walimu kusaidia serikali kuyaelezea mambo makubwa yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kutoka ushauri wenye hoja za kujenga kwa viongozi wa Chama na Serikali katika maeneo wanayoishi ili kuhakikisha ilani ya CCM inatekelezwa ipasavyo kwa maslahi ya wananchi.

Ryata amewapongeza walimu hao kwa umoja na uamuzi wao mzuri wa kuunda na kujiunga katika jukwaa la Walimu Wazalendo huku akisema Mwanachama au Kada wa CCM asipokuwa Mzalendo hawezi kuwa na tija ndani ya CCM na hawezi kufaidika vyema na fursa mbalimbali ndani ya Chama hicho na nchi kiujumla.

Sambamba na hilo, Ryata amewataka walimu hao kuendelea kuielimisha jamii na kusimamia maadili, misingi ya utoaji Elimu Bora na Malezi kwa watoto ambao ndio wanafunzi wao wanapokuwa shuleni.

Kwa upande wao walimu wazalendo wamekipongeza chama cha Mapinduzi (CCM)mkoa wa Iringa kuendelea kuwapa ushirikiano na kutambua mchango wao katika jamii huku wakiomba Uongozi uzidi kuwapambania na kuzisema kero na changamoto zinazowakabili walimu katika utumishi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...