Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema Serikali ipo katika hatua za mwanzo za maandalizi ya ujenzi wa daraja la mto Athumani lililopo wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.

Akijibu swali bungeni leo, Mhe. Kasekenya amesema katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25, Serikali imepanga kujenga na kukamilisha daraja hilo ili kunusuru maisha ya wananchi wa maeneo hayo hususan nyakati za mvua.

Amesema ujenzi huo unazingatia umuhimu wa daraja hilo linalounganisha barabara inayoelekea katika kiwanda cha magadi ambacho kipo kwenye hatua za ujenzi na kikikamilika kitatoa fursa za kiuchumi.

“Niwahakikishie wabunge na Wananchi wa eneo husika kwamba daraja la mto Athumani limepewa kipaumbele na Serikali na tayari Wizara imeshapeleka maombi ya fedha za ujenzi wa daraja hilo pamoja na madaraja mengine madogo kumi na tatu, ” amesisitiza Naibu waziri Kasekenya.

Naibu Waziri Kasekenya alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Zaytun Seif Swai alietaka kujua ni lini Serikali itaanza ujenzi wa daraja la Mto Athumani mkoani Arusha.

Daraja la Mto Athumani lipo katika barabara ya mkoa (Reginal Road) ya Mto wa Mbu-Selela-Engaruka-Ngaresero-Sale-Wasso-Loliondo yenye urefu wa (KM 217), katikati ya Kijiji cha Selela na Engaruka mkoani Arusha.

IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI

WIZARA YA UJENZI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...