Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania kupitia Kanda ya Ziwa imetoa elimu ya bima kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoani Mwanza ambapo jumla ya watumishi wapatao 26 wameshiriki mafunzo hayo.

Mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwemo Majukumu ya TIRA, Dhana ya Bima, Bima za Magari, Taratibu za madai, Umuhimu wa kuwa wakala wa bima na bima za Nyumba. Aidha, mafunzo hayo yamefunguliwa na Mkuu wa Takukuru Mkoani hapa Kamanda James Ruge na kuhitimishwa na Naibu Kamanda Idrisa Kisaka.

Mafunzo yaliyotolewa ni muhimu katika kutekeleza Mpango Mkakati wa Utoaji Elimu Kitaifa NIES ambapo TAKUKURU ni miongoni kwa Taasisi mojawapo ya kimkakati TIRA KWA SOKO SALAMA LA BIMA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...