Halmashauri ya mji wa Njombe mefanikiwa kutoa chanjo ya Saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri kati ya 9 - 14 kwa 91% na kuvuka lengo la angalau 80% kitaifa huku wakitarajia kufikia 100% ifikapo Mwezi Disember 2024 mwaka huu ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.

Simon Ngassa ni mtaalamu wa afya ambaye ni mratibu wa chanjo wa halmashauri hiyo akizungumza na vyombo vya habari amesema licha ya changamoto kadhaa walizopitia katika zoezi hilo lakini wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa chanjo kwa mabinti wengi kupitia shuleni na mikutano ya hadhara baada ya elimu kutolewa.

"Halmashauri ya mji Njombe tumefanikiwa kufikia 91% na kuvuka lengo lile ambalo tulikuwa tumepewa angalau 80% kitaifa hivyo tunaendelea kutoa huduma,na hawa ambao wataendelea kupata kwenye utaratibu wa kawaida ni matarajio yetu inapofika mwezi Desember mwaka huu nao wataingia kukamilisha asilimia hizi ambazo zimebaki"amesema Ngassa

Aidha Ngassa amesema halmashauri bado ina chanjo za kutosha ambapo ametoa wito kwa walengwa kuendelea kufika kwenye vituo vya afya kwa ajili ya chanjo hiyo.

"Tunatoa wito kwa wazazi kwamba huduma hii ya kutoa chanjo inaendelea kwenye vituo vyetu kwa wasichana wale ambao hawakuweza kupata chanjo ili inapofika mwezi Disember wasichana wote wawe wamekingwa dhidi ya saratani ya mlano wa kizazi kwa hiyo chanjo zipo kwenye vituo vyote vya kutoa huduma za afya"aliongeza Ngassa


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...