Na Fauzia Mussa Maelezo.05.05.2024.

Mkuu wa Oganaizesheni Afisi Kuu ya chama cha mapinduzi Zanzibar Omar Ibrahim Kilupi amezitaka jumuiya za chama cha Mapinduzi kuweka mikakati ya kuwatambua vijana ambao hawajasaliliwa katika datfari la wapiga kura ili waweze kusajiliwa.

Akifungua kongamano la jumuiya ya wazazi wa Mkoa wa Magharibi Kichama huko Skuli ya Ali Hassan Mwinyi Bububu amesema kuna baadhi ya vijana hawakujiandikisha katika awamu iliopita hivyo ni vyema kuwatambua na kuwahamasisha kujiandikisha katika awamu ijayo.

Amezitaja baadhi ya sababu zilizopelekea vijana hao kutojisajili kuwa ni pamoja na kutotimiza umri wa miaka 18 pamoja na kuwa mbali na vituo vya kujiandisha kwa kipindi hicho.

Aidha amezitaka jumuiya hizo, kuhakikisha vijana wote waliotimiza vigenzo wanajisajili ili kuweza kupata vijana wengi watakaoendelea kukiweka madarakani chama cha Mapinduzi ifikapo 2025.

“Kuna kundi la wananchi ambao wana sifa za kujisajili lakini hawajaenda kujisajili na kama tunavyojuwa kama hukujisajili katika daftari la kudumu la wapiga kura hutoweza kupiga kura, tuendeni tukahamasishe ili tusije kumuacha mtu nyuma.” alisema Kilupi.

Aidha amesema lengo la mafunzo hayo ni kutoa elimu ya uchaguzi na mmongonyoko wa maadili na kuwataka kuyafanyia kazi mafunzo walipopewa sambamba na kuwa mabalozi wazuri kwa wenzao.

Kwa upande wake Mlezi wa Mkoa wa magharibi kichama ambae pia Mwakilishi wa viti maalum kupitia jumuiya ya wazazi mkoa wa kusini Unguja Mhe. Sabiha Filfil Thani amesema kuna kila sababu ya Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuendelea kubaki madarakani katika Uchaguzi unaotarajiwa kufanyika hapo mwakani kutokana na kutekeleza kwa vitendo ilani ya chama hicho.

“Ilani ya CCM ilimtaka rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kujenga madarasa 1,500 kwa Skuli za Unguja na Pemba ambapo amevunja rikodi kwa kujenga madarasa 2273 sawa na silimia 150 ya malengo ya ilani ya chama cha Mapinduzi.” amefahamisha Mlezi huyo.

Katika kongamano hilo mada mbili ziliwasilishwa na kujadiliwa ikiwemo mmongonyoko wa maadili na uchaguzi Mkuu ambapo Kauli mbiu ni ”USHINDI WA CCM 2024-2025 JUMUIYA YA WAZAZI TUPO MSTARI WA MBELE”







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...