Hospitali ya Taifa Muhimbli-Upanga na Mloganzila imeendelea kuandika historia Afrika Mahariki na Kusini mwa Jangwa la Saraha katika matibabu ya ubingwa bobezi kwa Kupandikiza Uloto kwa wagonjwa waliokuwa na saratani ya damu.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Prof. Mohamed Janabi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu huduma ya Upandikizaji Uloto, zoezi lililoenda sambamba na kuruhusiwa kwa wagonjwa watano ambao wamepata huduma hiyo ambapo kwa sasa imefikisha jumla ya wagonjwa 16 tangu kuanzishwa kwa huduma hii Novemba 2021, idadi inayoifanya Muhimbili kuendelea kuongoza kwa matibabu hayo Kusini mwa Jangwa la Sahara.

“Tunapenda kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji uliofanywa wa miundombinu, kusomesha wataalam, ununuzi wa vifaa tiba ambavyo vimewezesha kutoa matibabu haya hapa nchini na kuwapunguzia wananchi gharama za kwenda nje ya nchi kutafuta matibabu ya kibingwa” ameongeza Prof. Janabi

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi MNH, Dkt. Mbonea Yonaz amesema huduma ya kupandikiza uloto inatolewa kwa mara ya tatu, kufanikiwa kwa upandikizaji huu kunatoa taswira ya mafanikio na mageuzi makubwa yanayoendelea katika sekta ya afya hapa nchini.

Dkt. Mbonea amebainisha kuwa wataalam wanafurahishwa sana pale wanapofanikisha matibabu ya ubingwa bobezi ikiwemo upandikizaji wa uloto kwa kuwa yanahitaji weledi, dawa na miundombinu wezeshi bora na yenye teknolojia ya kisasa duniani.

Naye, Deogratias Mwolo ambaye ni mmoja kati ya waliopandikizwa Uloto ameipongeza Serikali, uongozi wa hospitali na wataalam kwa kuwezesha kupata matibabu ya kupandikizwa hapa nchini huku wataalam wakitoa huduma bora na nzuri.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...