WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema michezo ni zaidi ya afya na burudani, ni fursa ya ajira na pia hupunguza magonjwa mwilini.

“Kama mnavyofahamu, michezo ni zaidi ya afya na burudani lakini leo tunathibitisha kuwa baada ya mbio hizi, sote tumefurahi na miili yetu imeimarika.”

Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Mei 11, 2024) wakati akizungumza na viongozi, wananchi na washiriki waliohudhuria hafla ya kufunga hafla ya TULIA MARATHON iliyofanyika kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.

Amesema kwa mujibu wa Wizara ya Afya, michezo inawezesha watu kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza. “Taarifa za Wizara zinasema kuwa nchi yetu inakabiliwa na changamoto ya ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza kama vile shinikizo la damu, kisukari, kiharusi na maumivu ya viungo kama magoti na mgongo. Kwa hiyo tujenge tabia ya kufanya mazoezi, ” amesema.

Amesema hivi sasa fedha nyingi zinatumika kutibu maginjwa hayo iwe ni kwa Serikali au mtu mmoja mmoja na kwamba magonjwa hayo yanaendelea kupoteza nguvukazi ya Taifa.

Ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuboresha michezo na hivyo kuongeza hamasa ya kitaifa ya kupenda michezo. “Sote tunakumbuka kuwa alianzisha mpango wa goli la Mama, akaanzisha changizo la Kitaifa kwa ajili ya timu za Kitaifa na hii inaenda sambamba na michezo ijayo ya AFCON 2027.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii izitumie mbio za Tulia Marathon kutangaza utalii wa mkoa wa Mbeya na mikoa iliyo jirani. “Mkoa huu una vivutio vingi na mikoa ya jirani inavyo vivutio mbalimbali. Tumieni mbio hizi kuwa fursa ya kutangaza utalii. TANAPA wekeni banda hapa, onesheni kuna vivutio gani kwenye mkoa huu na mikoa ya jirani,” amesema.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...