Katika kupambana na udumavu mkoani Njombe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe imeendelea kufikisha ujumbe kwa jamii kwa namna mbalimbali na sasa ni zamu ya Bajaji kufikisha ujumbe huo kupitia Mabango.

Bwana Chrispin Kalinga kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe amesema lengo la kuweka mabango hayo ni kufikisha ujumbe kwa jamii na Bajaji ni miongoni mwa chombo cha usafiri kinachotumiwa na watu wengi hivyo anaamini ujumbe huo utafika kwa jamii.

"Bajaji inatumiwa na makundi mbalimbali na rika tofuati tofauti na unafahamu hapa mjini Njombe na pale Makambako wananchi wanatumia sana usafiri wa Bajaji kwahiyo tunaamini kwa njia hii ujumbe utawafikia na adhma ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka ni kuona udumavu unaisha ndani ya mkoa wetu" amesema Kalinga.

Baadhi ya Madereva Bajaji mjini Njombe wamesema hatua ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuwashirikisha kupeleka ujumbe wa Lishe ni hatua nzuri kwani inaonesha serikali inatambua Bajaji ni moja ya sehemu inayohudumia watu wengi na itarahisisha ujumbe huo kufika kwa wananchi.

Kwasasa Kampeni ya Lishe mkoani Njombe inabebwa na kaulimbiu inayosema "Kujaza Tumbo Sio Lishe Jali Unachokula/ Unachomlisha" ikilenga kuhamasisha jamii kuzingatia lishe bora kutokana takwimu za matokeo ya awali ya utafiti wa hali ya afya nchini zilizotolewa na Ofisi ya Takwimu Nchini (NBS) 2022 kuonesha mkoa huo bado una changamoto ya udumavu kwa asilimia 50.4, huku mkoa wa Iringa ukiongoza kwa asilimia 56.9.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...