Mwandishi wa kitabu cha “And the Children Shall Lead Us”  Barry Childs (katikati) akionyesha nakala ya kitabu hicho katika  hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar e salaam hivi karibuni,wengine kwenye picha kushoto ni Mratibu wa mradi wa Africa Bridge  Kelvin Ngonyani  kulia ni mwandishi mwenza wa kitabu hicho, Philip Whiteley.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
SHIRIKA la kuhudumia watoto walio katika mazingira magumu Africa Bridge limeweza kuwasaidia watoto 7,700 katika kata sita na vijiji 37 katika mkoa wa Mbeya wilaya ya Rungwe kwa kuwasaidia na elimu, malazi na afya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wiki iliyopita kwenye uzinduzi wa kitabu cha “And the Children shall Lead Us” mtunzi wa kitabu hicho Barry Childs alisema kwamba alirudi Tanzania baada ya miaka 35 na kuumizwa na hali aliyoikuta ya watu wa maeneo ya vijijini na kuamua kuanzisha shirika hilo la kutoa msaada.

“watu ambao wengi nilikua nao katika Mkoa wa Arusha kati ya 1944 hadi 1962 nilikuta hali zao bado ni duni na wengine walikuwa wameshapoteza maisha kutokana na umasikini wa kutupwa na nikaamua kuandika kitabu hiki ili kuleta mtazamo chanya wa kuweza kusaidia watu wa vijini hasa watoto,” alisema.

Alisema, muundo unaotumiwa na shirika hilo la Africa Bridge ni aina mbili kwanza kushirikisha watoto wenyewe na wazazi na pia kushirikisha jamii husika kupitia kwenye kamati za vijiji ili kuweza kusaidia katika malezi ya watoto kuanzia shule, nyumbani na kwenye jamii kwa ujumla.

Childs aliongeza kwamba kupitia mradi huo watoto wanajifunza shughuli za ujasiriamali kama vile kufuga ngo’mbe, kukamua maziwa na kuuza na upandaji na ulimaji wa zao la parachichi kwa ajili ya biashara,

Aliongeza kwamba utunzi wa kitabu hicho na uanzishwaji wa mradi huo unatokana na tafiti iliyofanywa na Chuo Kikuu Texas nchini Marekani kupitia kituo chao cha Utafiti cha Ray Marshall na kusema mfumo unaotumiwa na mradi utaleta matokeo chanya nchini Tanzania.

Kwa upande wake , Mratibu wa mradi huo, Kelvin Ngonyani alisema kwamba kitabu hicho chenye simulizi la kusisimua na kinacholenga kuwatoa watoto kwenye umasikini na kuwapa maarifa ya kilimo endelevu, ujasiriamali na kuboresha maisha yao hasa maeneo ya vijijini.

Aliongeza kwamba mfumo wa kuwahudumia watoto ni kwa kupitia kamati familia na jamii kwa kiwashirikisha viongozi wa kata, mitaa na vijiji ili kuweza kuleta ufanisi katika kutoa msaada wenye matokeo chanya kwa mtoto kuanzia malazi na elimu yao.

Mmoja wa wanufaika wa mradi huo , kutoka Mbeya wilaya ya Rungwe ni Sara Mosses (22) ambaye kwa sasa anasoma Chuo cha Rungemba Mafinga na anachukua Stashada ya Maendeleo ya jamii ambaye alisema....mie ni mmoja wa wanaufaika na mradi huu kwa kusomeshwa kupitia zao la parachichi kuanzia shule ya msingi, sekondari na kwa sasa nachukua stashada ya Maendeleo ya jamii na nataka kurudi kuendelea kuhudumia jamii yangu hasa watoto ambao wako kwenye mazingira magumu hapa nchini,”

Mtunzi wa kitabu hiki kinachoitwa “And the Children Shall Lead Us” (Na Watoto Watatuongoza) Barry Childs, ambaye alikulia Tanzania na baadaye alikwenda kusoma Shahada ya Sayansi katika Saikolojia katika Chuo Kikuu cha KwaZulu-Natal Afrika kusini.

Childs alifanya kazi kwa miaka 17 katika kampuni ya Exxon na baadaye alikuwa Mkurugenzi wa Masomo katika Maabara ya Abbott. Baada ya miaka 35 akiwa nje ya nchi, Childs ameamua kurudi Tanzania ili kuendeleza ndoto yake ya kuwatoa watoto kwenye umaskini.


Sehemu ya kitabu chake inasema kwamba aliporudi nchini alikuta watu wakipambana na umasikini na athari za ugonjwa wa Ukimwi, hivyo aliamua kujipanga akiwa kwenye shirika la Abbot 2000 na kuanzisha mradi unaoitwa ‘Africa Bridge’ kusaidia watoto wa Kitanzania.

Kitabu hiki chenye kurasa 168 kimechapishwa kwa lengo la kushirikisha jamii kwa jumla juu ya mafanikio ya mradi wa Africa Bridge katika kuleta uzoefu katika utafiti ya kitaaluma na kuzidisha uelewa kwa jamii juu ya uwezo wake mkubwa wa kuwainua watoto walio hatarini zaidi kutoka kwenye umasikini.

Childs aliamua kuanzisha mradi wa Africa Bridge ili kuionyesha dunia namna bora ya kutumia rasiliamali zilizopo kama ardhi na kilimo ili kuweza kumwinua mtoto wa Kitanzania na jamii kwa jumla kuondokana na umasikini.

“And the Children Shall Lead Us” kinaelezea jinsi mradi wa Africa Bridge unavyofanya kazi, ulivyotokea na kutekelezwa, na yale yaliyofunzwa katika miaka 23 ya uendeshaji wake.

Childs, ambaye ni mwanzilishi wa Africa Bridge, aliishi miaka yake ya utotoni Tanzania na alimua kurudi baadaye kujitolea kusaidia nchi yake ya asili.

Kitabu hiki, kinachokusudiwa kuwa somo pendekezi katika Sayansi za Jamii, kinaelezea simulizi la kuvutia la mradi wa Africa Bridge, shirika la jamii la pekee, ambalo limeendeleza mfano wa kujitegemea unaokubalika wa kuinua jamii za watu wa vijijini Afrika kutoka katika umaskini uliopitiliza.

Mwanzilishi wake Bw Childs anaamini kwamba ili kubadilisha maisha ya watoto walio hatarini, mtiririko salama wa mapato ni muhimu kwa kuwaendeleza, kupata elimu, na kutoa fursa halisi za kuwawezesha kufikia malengo yao.

Africa Bridge ilianzisha vyama vya ushirika vya kilimo na kamati za watoto na za kuwainua wanawake wa vijijini kwa kuwawezesha kwa vitendo ili kuzalisha mapato endelevu huku wakikidhi mahitaji ya jamii.


Mwanzilishi wa Mradi wa Africa Bridge na mtunzi wa Kitabu cha ‘And the Chidren Shall Lead Us, chenye simulizi ya kuwatoa watoto kwenye umasikini na kuwapa maarifa ya kilimo endelevu, kuboresha maisha yao, Barry Childs (katikati) akikata utepe kuzindua kitabu hicho kupitia mradi wa Africa Bridge nchini, hafla ya uzinduzi huo imefanyika jijini Dar es Salam.
Mwandishi wa kitabu cha “And the Children Shall Lead Us,  Barry Childs akielezea historia ya maisha yake nchini Tanzania na sababu ya kuandika  kitabu hicho.
Mwandishi wa kitabu cha “And the Children Shall Lead Us”  Barry Childs akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Bodi wa mradi wa Africa Bridge nchini,Baraka Mtunga wakati wa hafla  hiyo.
Baadhi ya washiriki  wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa hafla hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...