KAMPUNI ya Airtel Tanzania inaendelea kushirikiana na tasnia ya nchini kwa ufadhili wa hivi karibuni wa Mkutano wa Kitaifa wa Maendeleo ya Sekta ya Habari uliohudhuriwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan aliyekuwa mgeni rasmi.

Katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam, Rais Samia alivipongeza vyombo vya habari kwa mchango wake mkubwa wa kuhabarisha umma juu ya hali ya maendeleo nchini.

“Vyombo vya habari vinafanya kazi kubwa kuhabarisha, kuelimisha na kuamsha jamii kuhusu mambo muhimu. Na kupitia kwao, serikali inapata kujua na kukusanya maoni ya umma kuhusu masuala mbalimbali. Sekta hii inahamasisha upatikanaji wa ujuzi mpya na maendeleo ya teknolojia kwa ustawi wa jamii zetu. Vyombo vya habari pia vinachangia kujenga uwajibikaji ndani ya sekta ya umma,” alisema.

Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka Airtel Tanzania, Beatrice Singano, alieleza kuwa vyombo vya habari ni sekta muhimu inayoendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya sekta ya mawasiliano na kutumia nguvu ya teknolojia kupitia majukwaa ya kidijitali.

"Vyombo vya habari vinasaidia kwa nafasi kubwa katika ukuaji wa maendeleo ya sekta tofauti. Ni sekta inayotoa taarifa kwa umma kuhusu bidhaa zetu ambazo zimeundwa kukuza maendeleo na ushirikishwaji wa kifedha lakini pia, inaonyesha mwelekeo wa sekta hii katika kiwango cha kimataifa," alielezea.

Aliongeza zaidi “Hivi majuzi tulizindua mradi wetu mkukwa unaoitwa Airtel SMARTWASOMI ambao umeundwa kushirikiana na serikali kukuza ujuzi na viwango vya wasomi wetu walioko shule za sekondari kuwa na uwezo wa kuja kufanya mambo mengi kidijitali. Tusingeweza kufikia shule nyingi kama tulivyofanya bila ushirikiano wa vyombo vya habari. Tutaendelea kusaidia sekta ya vyombo vya habari kwa njia bora tuwezavyo.”

Singano aliendelea kusema kwamba Airtel Tanzania imejizatiti kuimarisha na kupata mawasiliano kufuatia uanzishaji wa hivi karibuni wa Mkongo unaopita chini ya bahari wa 2Africa, ambao inaipa sekta ya kidijitali sura mpya ya maendeleo.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...