Angela Msimbira, KIGOMA

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Zainab Katimba amemuagiza Mkandarasi M/s CRJE East Africa LTD kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa barabara Wafipa - Kagera na Bangwe- Burega kwa wakati.

Mhe. Katimba ametoa kauli hiyo Mei 31, 2024 wakati alipokagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata ya Bongwe, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, mkoani Kigoma.

Amemtaka Mkandarasi kufuata sheria, taratibu na miongozo iliyowekwa kwenye mikataba ambayo inaeleza wazi barabara hiyo inatakiwa kukamilika lini ili wananchi waweze kupata huduma za usafirishaji.

Wakandarasi mnapopatiwa kazi jukumu lenu ni kutekeleza kwa mujibu wa ratiba iliyowekwa kwa kuwa mnapokuwa nyuma ya ratiba mnakwamisha maendeleo ya wananchi.

Amemtaka kuhakikisha kazi inakamilika kwa wakati kwa kuwa wananchi wanamatarajio makubwa na Serikali inahitaji kuona fedha inayotengwa kwa ajili ya ujenzi inaleta matokeo chanya.

Aidha amesema Serikali haitafumbia macho ucheleweshaji wa ujenzi wa miundombinu ya barabara ama kusuasua kwa utekelezaji wa miradi nchini.

Naye Diwani wa Kata ya Bangwe Mhe. Hamis Besere amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya trioni 11 kwa ajili utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Kigoma.

Aidha, amewaomba wakandarasi wanaojenga miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo kujenga kwa ubora unaotakiwa na kuikamilisha ndani ya muda wa makubaliano.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...