BALOZI wa Tanzania nchini Korea, Togolani Edriss Mavura ameambatana na wasanii aliowaalika kufanya ziara nchini Korea kusini na kukutana na msanii mkubwa nchini humo Ye-Jin kwa lengo kuimarisha mahusiano na kubadilishana ujuzi katika soko la filamu na kubadilishana mawazo ya namna ya kuendeleza sekta hiyo kimataifa.

Aidha wamekutana na na watengeneza filamu wakubwa Cheol-ha Lee na Yohwan KIM.

Director Cheol-ha Lee amesema yupo katika maandalizi ya filamu itakayohusisha waigizaji wa kimataifa’International’ na angependa kupata muigizaji kutoka Tanzania kwa Afrika.

Katika kikao hicho wasanii hao wametoa mawazo mbalimbali ikiwemo Serikali kuweka nguvu katika kuinua wasanii wadogo ili kukuza na kuendeleza vipaji.

Aidha wamepokea mwaliko kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan, kuja Tanzania kuchagua maeneo mbalimbali ya kufanyia filamu zao na kisha kutembelea vivutio maridhawa vinavyopatikana Tanzania.

Wameshukuru kwa zawadi za shuka za kimasai walizovalishwa na kiongozi wa msafara Steve nyerere, msanii Irene Uwoya na Blandina Chagula (Johari).









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...