Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan azindua Rasmi Huduma za Usafiri wa Treni ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam - Morogoro hadi Dodoma, katika eneo la Stesheni Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Pugu Jijini Dare es Salaam wakati akielekea Dodoma kwa Usafiri wa Treni ya Kisasa ya (SGR). Mhe. Rais Dkt. Samia amezindua Rasmi huduma za Usafiri wa Treni ya Kisasa (SGR) kuanzia eneo la Kilometa 0 Stesheni Jijini Dar es Salaam- Morogoro hadi Dodoma tarehe 01 Agosti, 2024.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua safari za Treni ya Kisasa (SGR) kuanzia eneo la Stesheni Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam hadi Dodoma tarehe 01 Agosti, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Masanja Kadogosa mara baada ya kuwasili Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR) Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akinyanyua juu Bendera na kushusha chini (Flag off) kuashiria uzinduzi rasmi wa safari za Treni ya Kisasa ya Umeme (SGR) katika eneo la Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam hadi Dodoma tarehe 01 Agosti, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua jengo la Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR) katika eneo la Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2024.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...