Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki kwenye mjadala (round tables discussion) kuhusu Kilimo barani Afrika, katika Mji wa Des Moines, Iowa nchini Marekani tarehe 30 Oktoba, 2024. Mjadala huo ambao uliandaliwa na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka barani Afrika, Serikali na Sekta binafsi ya Marekani hususan waliopo kwenye sekta ya kilimo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye mjadala (round tables discussion) kuhusu Kilimo Barani Afrika pamoja na Nishati Safi ya Kupikia katika Mji wa Des Moines, Iowa nchini Marekani tarehe 30 Oktoba, 2024. Kushoto ni Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinumwi Adesina akimsikiliza. Rais Dkt. Samia alishiriki mjadala huo kando ya mjadala wa Kimataifa wa Norman E. Borlaung ambao umeandaliwa na Taasisi ya World Food Foundation
Viongozi mbalimbali wakifuatilia mjadala kuhusu Kilimo Barani Afrika katika Mji wa Des Moines, Iowa nchini Marekani kando ya mjadala wa Kimataifa wa Norman E. Borlaung ambao umeandaliwa na Taasisi ya World Food Foundation tarehe 30 Oktoba, 2024.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...