Na Khadija Kalili Michuzi Tv
KAMATI  ya Olimpiki Tanzania (TOC) imeipongeza nchi ya Uturuki kwa kuwapatia Mkufunzi aliyetoa mafunzo kwa walimu wa mchezo wa Judo nchini.

Makamu wa Rais (TOC) Henry Tandau amesema hayo wakati akifunga mafunzo ya walimu wa mchezo huo yaliyofanyika kwenye shule ya Filbert Bayi.

Tandau amesema kuwa mafunzo hayo yameendeshwa na mkufunzi mwenye uwezo mkubwa na kuwapati mbinu nzuri walimu wa mchezo huo.

Kwa upande wake Katibu wa (TOC) Filbert Bayi amesema kuwa walimu hao wazingatie mafunzo hayo ili kuendeleza mchezo huo kupitia mashuleni.

Rais wa chama cha Judo nchini (JATA) Zaidi Omary amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa mchezo wa judo.

Akisoma risala ya washiriki wa mafunzo hayo Geophrey Mtawa amesema kuwa wanaiomba serikali kuwapatia magodoro na mafunzo ya mara kwa mara.

Mafunzo hayo ya siku 10 yamesherikisha walimu 24 wa mchezo wa Judo kutoka Bara na Visiwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...