![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiIPTBw1C2zeJMotBxHuXCT5UFpo-Zc6ED4cHIsCV6vzl4AnZGLfYGXsQg0CIs8xdghtgXGD18UE9atWCx3cyCsXty_HkngFAm3mbkr0A29cVs-UICjPsLTG1BW8Hn_qKLwZVgVwYkCiPvo49VJjhmC_T4q3ZNr7etn5eK1D_IR8q3yc292ULCzJaYNdxI/w640-h384/WhatsApp%20Image%202024-12-16%20at%206.23.49%20PM.jpeg)
MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kodi Mtwara, Maimuna Khatib leo Desemba 16, 2024 ameongoza timu ya maofisa wa kodi kutoka TRA Dar es Salaam kuwatembelea walipakodi wa Masasi kwa lengo la kuwashukuru kwa kulipa kodi kwa hiyari sambamba na kuwasikiliza changamoto zao kwa lengo la kuzitatua.
Maimuna amesema hatua hiyo inakuja ikiwa ni katika kutekeleza agizo la Kamishna Mkuu la kuwashukuru na kuwasikiliza walipakodi.
Aidha, Maimuna ametumia nafasi hiyo pia kuwakumbusha walipakodi kufanya malipo ya kodi zao awamu ya nne mapema kabla ya tarehe 31 ya mwezi huu wa Desemba ili kuepusha usumbufu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...