Mjumbe wa Halmshauri kuu ya chama cha Mapinduzi taifa MNEC Richard Kasesela amesema kuwa mwaka wa 2025 utakuwa mwaka wa kutenda haki kwa kila jambo na kwa kila mwananchi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi pamoja upendo na utu kwa kila mwananchi.
Na Fredy Mgunda
Mjumbe wa Halmshauri kuu ya chama cha Mapinduzi taifa MNEC Richard Kasesela amesema kuwa mwaka wa 2025 utakuwa mwaka wa kutenda haki kwa kila jambo na kwa kila mwananchi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi pamoja upendo na utu kwa kila mwananchi.
MNEC Kasesela alisema kuwa mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi kwenye vyama vya siasa hadi uchaguzi mkuu wa kuwapata madiwani, wabunge hadi Rais hivyo ni bora ikatumika haki katika chaguzi zote.
Alisema kuwa vyombo vyote vya dola na wananchi wakitenda haki na wakitendewa haki hakutatokea vurugu kama ambavyo zinavyotokea nchi za jirani mara baada ya uchaguzi.
MNEC Kasesela alisema kuwa kila mwananchi akiwa na nidhamu kwenye maamuzi ya kutenda haki na nidhamu ya fedha na muda basi Tanzania itanufaika sana na mwaka 2025 kwa kutenda haki.
Alimalizia kwa kuwaomba viongozi wa dini nchi nzima kuwaombea viongozi wa serikali na vyama vya siasa kudumisha amani, utulivu katika uchaguzi za vyama na uchaguzi mkuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...