NA MWANDISHI WETU, SIMIYU
ASKARI wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa kushirikiana na wenzao wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Jeshi la Polisi Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu, wamemuua fisi katika Kijiji cha Kimali ambaye alikuwa akiwasumbua wakazi wa eneo hilo.

Fisi huyo aliyeuawa anadaiwa kuwa na alama ya jina la mtu upande wa paja lake la kushoto, huku akiwa na shanga shingoni.

Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Anna Gidarya amewataka wananchi wote wilayani humo wanaomiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria kuzisalimisha haraka kwa wahusika wa uhifadhi, kabla ya hatua kali hazijachukuliwa dhidi yao.

Kumekuwepo na matukio ya fisi kushambulia watoto kuanzia majira ya saa moja usiku katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Itilima.

Takwimu zilizotolewa wilayani Itilima zinaonyesha kuwa kuanzia mwaka 2024 hadi sasa watu nane wamefariki dunia baada ya kushambuliwa na fisi na wengine 17 wamejeruhiwa, huku fisi 16 wakiuawa katika kipindi hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...