Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema kuwa Serikali inaendelea kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kulipatia vitendea kazi ambapo sasa inatekeleza mradi wa ununuzi vifaa mbalimbali vya kuzima moto na uokoaji pamoja na magari 150 ya kuzima moto na uokoaji.

Bashungwa ameeleza hayo tarehe 03 Februari 2025 wakati akijibu swali la Mbunge wa Ngorongoro, Emmanuel Shangai aliyetaka kujua Je, lini Serikali itanunua gari la Zimamoto Wilaya ya Ngorongoro.

“Kwa sasa Serikali inatekeleza mradi wa ununuzi vifaa mbalimbali vya kuzima moto na uokoaji pamoja na magari 150 ya kuzima moto na uokoaji” amesema Bashungwa

Amesema pindi magari 150 ya kuzima moto na uokoaji yatakapofika nchini, yatakayosambazwa nchi nzima ikiwemo Wilaya ya Ngorongoro.

Aidha, amesema Serikali inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeshaliwezesha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kununua magari 12 ya kisasa ambapo moja wapo lilitumiaka kuzima moto katika jengo gorofa la TRA Kariakoo.

Bashungwa amesema Serikali ipo mbioni kununua helikopta moja maalum kwa ajili ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambayo yataenda sambamba na kuwapatia Mafunzo Maafisa, Wakaguzi na Askari wa Jeshi hilo.

 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Innocent Bashugwa akijibu maswali katika Bunge linaloendelea Mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...