Na Khadija Kalili Michuzi TV
MKUU wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge amesema kuwa Mkoa wa Pwani utazindua Huduma ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia 'Samia Legal Aid' tarehe 24 Februari 2025 katika Viwanja vya Stendi ya zamani Mailimoja Kibaha.

RC Kunenge amesema hayo leo tarehe 22 Februari 2025 kwenye mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika ofisini kwake Mkoani hapa. Pia ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Pwani kujitokeza kwa wingi kesho Jumatatu kuanzia saa tatu asubuhi.

"Wananchi wote wenye malalamiko wajitokeze kupeleka malalamiko yao yanayohitaji msaada kisheria na nina imani watapata msaada" amesema Kunenge.

Amesema kuwa kwa malalamiko yote yanayohusiana na masuala na ndoa , mirathi, ardhi wote watasikilizwa

Huduma hii inatolewa na Wizara ya Katiba na Sheria.

Tayari Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia imefanyika kwenye Mikoa 19 na Pwani unakua Mkoa wa 20.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...