Na Mwandishi Wetu.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula ameshiriki Kikao Kazi cha Kimkakati cha Maafisa Utamaduni na Maafisa Maendeleo ya Michezo Tanzania akiwa sehemu ya wadau muhimu waliopewa dhamana ya kusimamia maadili katika Taaluma ya Habari nchini.
Moja ya mada zilizopewa kipaumbele katika Kikao Kazi hicho kilichozinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ni Mmomonyoko wa Maadili ya Mtanzania.

Kikao Kazi hicho cha siku 4 cha Mafundo na Mazingativu kilichoandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kinafanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam kuanzia leo tarehe 22 hadi 25 Aprili, 2025.
Mbali na kuwashirikisha Maafisa Utamaduni na Maafisa Maendeleo ya Michezo Kikao Kazi hicho kimewakutanisha Wakuu wa Taasisi na viongozi wa vyama vya Michezo, Sanaa na Utamaduni.
Kauli Mbiu ya Kikao Kazi hicho ni "Utamaduni, Sanaa na Michezo, Msingi wa Maadili ya Mtanzania, Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025".
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula (pichani) ameshiriki Kikao Kazi cha Kimkakati cha Maafisa Utamaduni na Maafisa Maendeleo ya Michezo Tanzania
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...