Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Kizito Mhagama, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wabunge Wawakilishi wa umoja wa Mabunge Duniani kutoka Tanzania, ameongoza msafara wa Wabunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa 150 wa Mabunge Duniani (IPU) unaoendelea mjini Kashkenti, Uzbekistan, kuanzia Aprili 5 mpaka 9, 2025.

Katika mkutano huu, Mhagama ameonyesha juhudi za Bunge la Tanzania katika kuisimamia serikali na kuhakikisha kwamba inatekeleza majukumu yake kikamilifu, hasa katika nyanja za maendeleo na haki za binadamu.

Mkutano huo unazungumzia nafasi ya Mabunge katika kupigania maendeleo na haki za jamii (Social Development and Justice), ambapo Bunge la Tanzania limekuwa na nafasi muhimu katika kuhamasisha na kutunga sheria zinazolenga kuboresha hali ya maisha ya wananchi.

Mhagama ameelezea hatua muhimu ambazo Tanzania imechukua katika kuimarisha maendeleo ya kijamii na haki za binadamu, akisisitiza umuhimu wa Mabunge duniani kushirikiana ili kufikia malengo ya pamoja ya maendeleo endelevu.

Huu ni mkutano wa kihistoria ambao umeipa Tanzania fursa ya kuonyesha mchango wake katika masuala haya ya kimsingi, huku ikiendelea kujenga mifumo bora ya utawala inayozingatia haki na maendeleo ya wananchi wake.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...